BLACK STONE YABEBA UBINGWA - LIGI YA PIKIPIKI KIMAMBA.
Kikosi cha BLACK STONE |
NA COSMAS DOSSANTOS
MOROGORO.
Klabu ya BLACKSTONE imewapa burudani ya nafsi mashabiki wake leo Baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KIMAMBA FIBRES katika mchezo wa hatua ya fainali ya ligi ya Pikipiki aina ya SANLG katika Uwanja wa Kimamba Secondary School maarufu kama Mabatini Studium.
Mpira ulianza kwa kasi baada ya timu hizo zote mbili kushambuliana kwa vipindi mpaka dakika ya 35 katika kipindi hicho cha kwanza lakini katika dakika ya 37 BLACKSTONE walionekana kuchangamka zaidi na kuonyesha kwa mashabiki wake kuwa wanatafuta kitu.
Katika kipindi hicho cha kwanza dakika ya 39 Mshambuliaji DULLA ZUNGU aliweza kuwanyanyua mashabiki na wapenzi wa BLACKSTONE kwa kufunga goli maridadi kabisa bila presha ya kusongwasongwa na walinzi wa KIMAMBA FIBRES baada ya mlinzi wa kati wa Timu hiyo AMIRI CHUMVI kufanya kosa la kuupiga mpira kichwa ambao haukwenda mbali ndipo Mshambuliaji wa BACKSTONE akaweza kuutendea haki mpira huo na kuuweka kimiyani.
Mpaka timu hizo zinakwenda mapumziko matokeo
yalikuwa BLACKSTONE anaongoza moja kwa bila
dhidi ya KIMAMBA FIBRES.
Mshambuliaji DULLA ZUNGU wa BLACKSTONE |
Hivyo bao hilo la pekee lilolofunga na mshambuliaji DULLA ZUNGU limewafanya BLACKSTONE kuwa mabingwa wa Ligi hiyo ya Pikipiki aina ya (SANLG) kwa mwaka 2017 katika Wilaya ya Kilosa, Tarafa ya Kimamba Mkoani Morogoro.
Na baada timu hizo kurudi uwanjani hali ya mchezo ilibadilika zaidi baada ya wachezaji wa KIMAMBA FIBRES kuonekana kupambana zaidi ili kutafuta goli la kusawazisha katika kipindi hicho cha pili. Lakini jitihada za timu hiyo zilionekana kugonga mwamba kwa safu ya Ulinzi ya BLACKSTONE kuwa makini zaidi na kukaba kwa kushirikiana tena kwa umoja wa hali ya juu .
BLACK STONE YABEBA UBINGWA - LIGI YA PIKIPIKI KIMAMBA.
Reviewed by Abdurazak Ngowo
on
September 22, 2017
Rating:
No comments: