JE! NI TIMU GANI KUTOKA KIFUAMBELE JUMAPILI HII.
MANCHESTER UNITED vs LIVERPOOL
|
Mbio za kugombania ubingwa wa Kombe la Premier League sasa
zimeshika hatamu na joto limepanda kwa mahasimu wawili Manchester United
na Liverpool ambao watachuana vikali pale Old Trafford Jumapili ya wiki
hii. Liverpool wanashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ya
Uingereza mpaka sasa nyuma ya vinara Chelsea na wanaingia kwenye mechi
hii wakiwa vifua mbele, lakini United nao wanaweza kupunguza tofauti ya
pointi iliyopo mpaka kubakisha mbili tu endapo watapata ushindi katika
mtanange huu.
Kazi iliyokuwa ikiotewa ndoto na Jose Mourinho ya kuinoa na kuiongoza Manchester united imegeuka kuwa ujinamizi baada ya kuanza kwa kusuasua na kuambulia suluhu tatu mfululizo mwezi Desemba, lakini ushindi mara sita mfululizo walioupata hivi karibuni umewafanya Mashetani hawa wekundu kupata matumaini ya kumaliza ligi ndani ya nafasi nne za juu msimu huu na huenda ikawa Zaidi ya matumaini haya kwa kumaliza nafasi nzuri Zaidi. Pande zote zimeshiriki mechi za kuwania Kombe la EFL hatua ya nusu fainali kabla hawajakutana pale Old Trafford lakini Klopp na Mourinho wote tayari watakuwa wameelekeza hisia zao katika mchezo huu ambao hakika utakuwa ni wa kusisimua na kukata na shoka mjini Salford! |
JE! NI TIMU GANI KUTOKA KIFUAMBELE JUMAPILI HII.
Reviewed by Abdurazak Ngowo
on
January 13, 2017
Rating:
No comments: